A-TOWN BALAA LINGINE!!!
SHEKHE
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Said Juma Makamba amejeruhiwa vibaya kwa kumwagiwa maji yanayohisiwa kuwa tindikali na watu wasiojulikana juzi usiku akiwa nyumbani kwake jijini Arusha.
Shekhe Makamba, ambaye amelazwa katika Wodi ya Majeruhi kwenye Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru, amejeruhiwa vibaya maeneo ya usoni, kifuani na mgongoni huku akiendelea na matibabu.
Akizungumza kwa tabu, shekhe huyo alisema tukio hilo lilitokea saa 5 usiku wa kuamkia jana nyumbani kwake kwa Mromboo Arusha, wakati akijiandaa kulala baada ya kutoka kuswali Swala ya Tarawei.
Shekhe Makamba ambaye pia ni Imamu wa Msikiti wa Sekei mjini Arusha, alisema baada ya swala hiyo alirejea nyumbani kwake akisindikizwa na vijana wawili ambao walikuwa wakiswali pamoja na kuingia ndani ya nyumba yake ili kulala.
Alisema hata hivyo, kabla ya kulala alikwenda kujisaidia katika choo cha nje na kwamba wakati akirudi ili aingie ndani akipitia nyuma ya nyumba ghafla alimuona mtu akiwa amesimama jirani na mlango.
Alieleza kuwa wakati akitaka kumwangalia zaidi alishtukia mtu huyo akiinua mkono na kumwagia maji yaliyompatia maumivu makali usoni na kifuani.
‘’Wakati natoka msalani nikipitia uwani kwangu niliona kama mtu ameinama pembeni yangu wakati najaribu kumsogelea ili nijue ni nani nilihamaki mtu huyo akinimwagia maji yaliyonisababisha maumivu makali sana yenye asili ya moto na ngozi kuanza kubabuka,’’ alisema shekhe huyo.
Aliongeza kuwa baada ya tukio hilo alianza kupiga kelele kuomba msaada ambapo majirani walijitokeza na kumpa msaada wa kumpeleka hospitali, kwa vile wakati huo macho yake yalikuwa hayaoni na wakati wote alikuwa akilia.
Pamoja na kujeruhiwa vibaya sehemu za usoni, kifuani na mgongoni, pia ana majeraha kwenye mikono na machoni na hali yake bado ni mbaya japo madaktari wanaendelea kumpatia matibabu.
Kaimu Katibu wa Bakwata Mkoa wa Arusha, Abdallah Masoud akizungumzia tukio hilo alieleza kushitushwa nalo akisema limefanana na lile la Katibu wa Bakwata Mkoa wa Arusha, Abdulaziz Jonjo ambaye mwaka jana alilipuliwa kwa bomu nyumbani kwake akiwa amelala.
Alisema kuwa matukio hayo yamekuwa yakijirudia huku wahusika wakishindwa kutiwa mbaroni na kudai kuwa matukio hayo yanahusiana na masuala ya kigaidi.
Aliongeza kuwa pamoja na kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi, lakini wamekuwa hawapati matunda ya kukamatwa kwa watuhumiwa ingawa alisema wanajulikana.
Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema polisi wameanza uchunguzi wa tukio hilo na kwamba taarifa zitatolewa pindi washukiwa watakapotiwa mbaroni kwani uchunguzi bado unaendelea na kwamba hakuna mtu anayeshikiliwa hadi sasa.
UKWELI HUU HAPA KUHUSU Agnes Gerad wa masogange
HUKU
skendo ya kunaswa akiwa na madawa ya kulevya ikiendelea kumtesa kwenye
mitandao mbalimbali ya kijamii, Video Queen maarufu Bongo, Agnes Gerald
‘Masogange’ anatarajiwa kupandishwa kortini nchini Afrika Kusini leo
kujibu shitaka ambalo mwenyewe hajaliweka wazi, Ijumaa linakupasha.
Agnes Gerald ‘Masogange’.
Na Mwandishi Wetu
HUKU skendo ya kunaswa akiwa
na madawa ya kulevya ikiendelea kumtesa kwenye mitandao mbalimbali ya
kijamii, Video Queen maarufu Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ anatarajiwa
kupandishwa kortini nchini Afrika Kusini leo kujibu shitaka ambalo
mwenyewe hajaliweka wazi, Ijumaa linakupasha.
Dawa za kulevya lakini siyo walizokamatwa nazo akina Agnes na Melisa.
AWALI YA YOTE
Mwishoni mwa wiki iliyopita, habari ya mjini ilikuwa Masogange kanaswa na madawa ya kulevya nchini Afrika Kusini.
Habari zilisambaa kwamba sanjari na Masogange, mwingine aliyenaswa naye
ni mdogo wake (mtoto wa mama yake mdogo Agnes) aitwaye Melisa Edward.
Kwa mujibu wa habari hiyo ya mjini, wawili hao walinaswa Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Oriver Tambo uliopo Kempton Park siku ya Ijumaa
wiki iliyopita wakitokea Tanzania wakiwa na ‘mzigo’ wa kilo nyingi aina
ya ‘crystal methamphetamine’ wenye thamani ya shilingi za Kitanzania
bilioni 6.8!
Melisa Edward aliyekamatwa na Agnes.
IJUMAA LAANZA KUSAKA UKWELI
Baada ya kunasa habari hiyo, Ijumaa
liliingia mzigoni kuusaka ukweli ambapo hata hivyo, madai hayo yalikuwa
yakijifungafunga sana.
Mtu mmoja wa karibu na Masogange alipoulizwa kuhusu ukweli au uongo wa habari hiyo alikuwa na haya ya kusema:
“Ni kweli Agnes amekamatwa akiwa na madawa ya kulevya kule Sauzi.
Lakini si yenye thamani hiyo ya bilioni sita bali ni milioni arobaini
tu. Hata hivyo, ameachiwa kwa dhamana ila paspoti yake imezuiliwa.
“Nadhani kuna mambo yanawekwa sawa ikiwezekana atarudi nyumbani.”
JIJINI DAR, KAMANDA WA KUPAMBANA NA MADAWA YA KULEVYA ANENA
Jumatatu iliyopita, Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Kudhibiti Madawa ya
Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa aliviambia vyombo vya habari kuwa,
Watanzania wawili walikamatwa nchini Afrika Kusini na mamlaka ya mapato
wakiwa na madawa ya kulevya kutoka Tanzania yenye thamani ya shilingi
bilioni 6.8.
Kamanda Nzowa aliwataja Watanzania hao kuwa ni Agnes
Gerald ambaye ana miaka 25 na Melisa Edward mwenye miaka 24. Alisema
wawili hao baada ya kukamatwa na chombo hicho walikabidhiwa kwa polisi
ambapo mahojiano yanaendelea.
IJUMAA LAMWIBUKIA KAMANDA NZOWA
Baada ya Kamanda Nzowa kuwataja
kwa majina wawili hao Jumatatu iliyopita, siku iliyofuata, Ijumaa
lilipiga hodi kwenye ofisi za kamanda huyo kwa lengo la kutaka kujua
kama Agnes Gerald aliyemtaja jana yake ni Masogage au majina yanafanana
tu.
Kamanda huyo hakuwepo ofisini kwake asubuhi hiyo na kwa mujibu
wa wasaidizi wake, alikuwa kwenye kikao cha dharura kwenye Ofisi za
Polisi wa Kimataifa ‘Interpol’.
APIGIWA SIMU
Ilibidi Ijumaa limsake kwa njia ya simu ya kiganjani
kwa mara kadhaa. Alipopokea akaulizwa kuhusu Agnes Gerald aliyemtaja
kama ni Masogange yule staa.
Kamanda Nzowa: “Eee, mimi siwezi kusema
ni huyo, ninachojua ni Agnes Gerald tu basi. Sasa kama ni Masogange
mimi sifahamu lolote.”
JUMANNE USIKU SIMU KUTOKA SAUZI
Mpaka hapo, timu nzima iliyokuwa ikifuatilia habari hiyo haikuona
ukweli wa Agnes Gerald kuwa ni Masogange na kwa vile siku zote Global
Publishers inasimamia utafiti kabla ya kuandika habari iliamua kuiweka
pembeni kwanza ili kuendelea kuichimba.
Saa 2:14 usiku wa siku hiyo,
Ijumaa lilipokea simu yenye kuashiria wito (code number) ni ya nje na
kabla haijapokelewa, ilibainika ni ya Afrika Kusini.
Ijumaa: Haloo.
Sauti: Haloo, mimi Masogange.
Ijumaa: Mambo Agnes, pole sana na mkasa uliokupata bwana, pole sana.
Agnes: Kwanza naumizwa sana na maneno ambayo watu wanazidi kuyaeneza
sehemu mbalimbali bila kuwa na uhakika wowote, mimi sikukamatwa kwa
sababu ya madawa ya kulevya.
“Mkasa nilioupata siyo ambao watu wanaueneza kwenye mitandao mbalimbali na katika vyombo ya habari.”
Ijumaa: Kwa hiyo madai ya kukutwa na madawa ya kulevya si ya kweli?
Agnes: Kweli nilikamatwa huku kwa matatizo f’lan ila siyo ishu ya madawa kama watu wanavyosambaza.
Ijumaa: Ni tatizo gani sasa?
Agnes: Unajua sipendi tena kuwapa watu faida ila lilikuwa ni tatizo la
kawaida, nilikamatwa na baada ya hapo nilitoka na niko huru. Nasubiri tu
kwenda mahakamani Ijumaa (leo) mara moja kisha n’tarudi Bongo.
Ijumaa: Mh! Sasa Egg, mbona huku mpaka viongozi wa polisi wamesema ni madawa?
Agnes: Hapana, siyo, ipo ishu ndogo tu.
Ijumaa: Haya pole sana kwa misukosuko.
Agnes: Asante sana, nitakuja huko siku si nyingi.
Habari hii imeandikwa na Imelda Mtema, Haruni Sanchawa na Musa Mateja.
HAPA MPAKA KIELEWEKE! (JOYCE KIRIA) AMTAKA MUMEWE
BAADHI YA PICHA ZIKIMWONYESHA MTANGAZAJI JOYCE KIRIA
AKILILIA HAKI YAKE YA MSINGI
Mtangazaji wa televisheni ya Chanel 5 EATV Joyce Kiria akiwa amewashikilia watoto wake Lingatone Kileo kulia na Lincorn wakati alipozungumza na waandishi wa habari katika mtaa wa Samora na kupaza sauti kuomba msaada kwa Rais Jakaya Kikwete na watanzania kwa ujumla ili kusaidiwa na kujua aliko mume wake Henry Kileo ambaye inadaiwa amepelekwa Igunga akituhumiwa na kesi huko Joyce Kiria amesema mpaka sasa hajaambiwa kama mume wake yuko wapi hivyo hata kama ana makosa anaomba afahamishwe kwani hajui kinachoendelea mpaka sasa
MNYAMA SOGY DOGY ATINGISHA GETI LA CHADEMA
Nguli wa muziki wa kizazi kipya Soggy Doggy Anter aka Anselm Tryphone Ngaiza leo ametangaza nia ya kugombea Ubunge wa jimbo la Segerea, Dar es Salaam kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, MWAKA 2015.
Msanii huyo ametiririka katika ukurasa wake wa facebook, na hapa nanukuu "Shikamoo Mbunge wa Segerea, Makongoro Mahanga, imetosha sasa nadhani ni zamu yangu kuwatumikia wana-segerea 2015 kupitia CHADEMA" mwisho wa kunukuu. Pia kwenye ukurasa wake wa twitter imesomeka ivyo ivyo.
Msanii huyu amesema ameamua kufanya ivi ili kuwasaidia na kuwaletea maendeleo wana-segerea na watanzania kiujumla.
Pia ameamua kugombea kupitia CHADEMA, kwasababu ndo chama kinachoweza kufanya mabadiliko kwenye jamii kwasasa.
Nikamuuliza je amemfuata rafiki yake Joseph Mbilinyi aka "SUGU" katika chama icho, akasema hapana, hawajawahi kupewa ushawishi wowote wa kisiasa na Nguli huyo wa muziki wa Hip Hop.
Wana-Segerea kazi kwenu kijana ameamua na amedhamiria
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiW2gKOy-YalEoj3ZsqNtcecUvE38nQJKApS-g7g_t4w_oSzDTEMZktFExAe9_zAGU6sQyCfcAvPbW5CdWqy_4e3Eo-RHA-mPm80nUBXXWEjARXSE-yH4sBlsKWDmepBUzfgryRMgEeW3jk/s1600/soggy+dogy.jpg)
No comments:
Post a Comment