Tuesday, 29 October 2013

USHINDI wa Timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 ‘Tanzanite Stars’ kwa kuifunga Msumbiji mabao 10-0 juzi Jumamosi umeipa rekodi timu hiyo.
Ushindi huo uimeifanya timu hiyo kuingia katika orodha ya timu zilizoshinda mabao mengi katika mashindano ya kimataifa au ya Bara la Afrika.
Kufuatia matokeo hayo ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia, Msumbiji inatakiwa kushinda zaidi ya mabao 10 ili kusonga mbele, jambo ambalo wengi wanachukulia kama linahitaji miujiza.
Wanawake wa Tanzania wanaingia katika rekodi ya miongoni mwa timu zilizovuna mabao mengi katika mashindano ya kimataifa au yale yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka la Afrika (CAF).
Timu ya wanawake ya Tanzania ingeongeza mabao mawili tu ingefikia rekodi iliyowekwa na Pamba ya Mwanza mwaka 1989 kwa kuwa timu ya kwanza ya Tanzania kushinda mabao mengi katika mashindano ya kimataifa au yale ya Afrika.
Pamba ya Mwanza iliweka rekodi hiyo baada ya kuifunga Anse Boileau ya Shelisheli mabao 12-1 katika mechi ya marudiano ya iliyokuwa michuano ya Kombe la Washindi Afrika iliyochezwa mwaka 1990 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Pia ushindi huo ulikuwa rekodi ya Afrika kwani hadi kufikia mwaka huo hakuna timu ya bara hilo iliyowahi kushinda kwa idadi kubwa ya mabao katika mashindano mbalimbali.
Pamba iliitoa Anse Boileau katika mwaka huo kwani katika mchezo wa kwanza uliochezwa huko Victoria, Shelisheli, timu hiyo iliibuka na ushindi wa mabao 5-0 na kuifanya kusonga mbele kwa mabao 17-1.
Kwa mujibu wa tovuti ya Televisheni ESPN, rekodi ya Pamba ilivunjwa mwaka 1994 na Mbilinga ya Gabon, ambayo iliicharaza Renaissance ya Chad mabao 13-0 katika mechi ya Kombe la Washindi barani Afrika mwaka 1994.
Pia rekodi za shirikisho la kimataifa linalojihusisha na historia na rekodi za soka zinaonyesha kuwa rekodi ya dunia inashikiliwa na Deportivo Arabe Unido ya Panama, iliyowahi kuichakaza Deportivo Jalapa ya Nicaragua 19-0 katika mechi ya Klabu Bingwa ya CONCACAF.
Rekodi za shirikisho hilo la kimataifa zinaonyesha kuwa Ajax Amsterdam ya Uholanzi inashikilia rekodi ya Ulaya baada ya kuiliza Red Boys Differdange ya Luxembourg katika mechi ya kwanza ya UEFA mwaka 1984.
Kwa bara la Oceania, timu ya Central United FC ya New Zealand ndiyo inayoshikilia rekodi baada ya kuilaza Lotoha’pai ya Tonga mabao 16-0 mwaka 1999.

MHESHIMIWA RAISI AHUTUBIA BARAZA KUU UN

  
New York. Rais Jakaya Kikwete juzi alihutubia kikao cha 68 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (Unga), New York, Marekani na kusema kama nchi tajiri duniani zingetoa fedha za kutosha kama zilivyokuwa zimeahidi, ni dhahiri kuwa dunia ingeweza kufanikisha utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo ya Milenia (MDG’s) na malengo yake yote katika kipindi cha miaka 15 kama ilivyokuwa imeamuliwa mwaka 2000.

Aidha, Rais Kikwete alisema Afrika haitochoka kudai haki ya kufanyika kwa mageuzi ya msingi ndani ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC), ili kuliwezesha bara hilo lenye idadi kubwa zaidi ya wanachama kwenye Umoja wa Mataifa (UN) kuwa na uwakilishi wa kudumu.
Katika hotuba yake ya dakika 15, Rais Kikwete alisema ni jambo lisiloelezeka kuwa dunia ya leo inaendelea kushuhudia umasikini wakati kuna raslimali na utajiri wa kutosha wa kumaliza tatizo hilo ikiwa kuna utashi wa kisiasa kumaliza tatizo hilo.
Rais Kikwete alikiambia kikao hicho ambacho mada yake kuu ilikuwa `Mjadala Kuhusu Ajenda ya Maendeleo Duniani baada ya mwaka 2015' kuwa pamoja na kwamba umasikini mkali zaidi duniani umepunguzwa kwa nusu katika kipindi cha utekelezaji wa MDG, bado zaidi ya watu bilioni 1.2 wanaishi katika mtego wa umasikini mkubwa.
Alisema kuwa mbali na watu hao, bado kiasi cha watoto wanaokadiriwa kufikia 19,000 chini ya umri wa miaka mitano na wanawake 800 hupoteza maisha kila siku kwa magonjwa ambayo yanaweza kuzuilika na kutibika.
“Hili ni jambo ambalo halikubaliki kabisa katika dunia iliyojaa neema ya kila aina tunamoishi leo ambako kuna maendeleo ambayo hayajapata kuonekana katika historia ya binadamu ya sayansi na teknolojia ambayo yanaweza kutumika kumaliza changamoto zote za maendeleo zinazokabili jamii ya binadamu sasa.
“Katika dunia ambako kuna chakula cha kutosha kumlisha kila mtu, hakuna sababu ya mtu yeyote kulala na njaa na kukabiliwa na ukosefu wa lishe. Katika dunia yenye utajiri mkubwa kama wa sasa, hakuna sababu kwa nini umasikini, njaa na dhiki viendelee kuleta dhiki na kusababisha shida kubwa kwa watu wengi kiasi hiki.”
Rais Kikwete alisisitiza: “Katika hali hiyo, ni jambo lisiloingia akilini kwa nini Malengo ya Milenia hayakufanikiwa kwa kiwango cha juu kabisa.
“Kama nchi tajiri na zilizoendelea duniani zingekuwa zimetoa fedha na rasilimali za kutosha kama ilivyokuwa imekubaliwa chini ya lengo la nane kwa mipango hiyo kwa mujibu wa makubaliano na ahadi zao katika mikutano ya nchi tajiri duniani ya G8 na G20, tungefanikiwa kutekeleza mipango hiyo,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:
“Kwa maana hiyo, litakuwa ni jambo la kujidanganya kama tulijadili nini tufanye kuhusu Malengo ya Maendeleo ya Milenia Baada ya 2015 bila kujadili na kukubaliana kuhusu jambo la msingi la jinsi ya kugharimia mipango hii.”
Mapema leo, Rais Kikwete amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon na baadaye alikutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani (anayeshughulikia siasa), Wendy R Sherman.

Friday, 18 October 2013







 ZITO BADO HAVIELEWI VYAMA




MWENYEKITI wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Kabwe Zitto, ameendelea kusisitiza kuwa hadi sasa hakuna chama chochote cha siasa kilichowasilisha ripoti ya ukaguzi wa hesabu zake kwa Msajili wa Vyama vya Siasa na kuvitaka vyama hivyo kuacha propaganda na kulichukulia suala hilo kisiasa.

Amesema hazungumzi suala hilo kama Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, bali anasimamia Sheria na kama hawataki, wamshauri Spika wa Bunge, Anne Makinda, avunje kamati yake.
“Napenda niwaambie nazungumzia suala hili si kama Naibu Katibu Mkuu wa Chadema bali Mwenyekiti wa PAC na ninasimamia sheria,” alisema.
Akizungumza jana katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam, Zitto alisema tangu atoe tamko la kutaka vyama hivyo vijiandae kujieleza kwanini havijawasilisha ripoti hizo za ukaguzi, amekuwa akisikia kelele tu na hakuna chama chochote kilichotekeleza kisheria jukumu hilo la kuwasilisha taarifa zake kwa Msajili tangu 2009 kama vinavyodai.                            “Najua kuna vyama vinajitetea kuwa tayari vimefanya ukaguzi wa hesabu zake, sasa kama kweli ziko wapi hizo ripoti, Sheria iko wazi, ukaguzi ukikamilika ripoti inatakiwa kuwasilishwa kwa Mkaguzi Mkuu na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG), na Msajili na si kuzifungia kabatini,” alisisitiza Zitto.</p>
Alisema amemuagiza Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, kuwaandikia barua ya kisheria viongozi wa vyama tisa vinavyopata ruzuku ya Serikali, ya kuwaita mbele ya kamati hiyo, Oktoba 25, mwaka huu ili kujieleza kwanini hawajawasilisha ripoti hizo kwa Msajili kwa kipindi cha miaka minne iliyopita.
Vyama hivyo ambayo vimeshakula Sh bilioni 67.7 bila kutoa ripoti ya matumizi yake ni CCM Sh bilioni 50.9, Chadema Sh bilioni 9.2, CUF bilioni 6.3, NCCR-Mageuzi Sh milioni 677, TLP Sh milioni 217, UDP Sh milioni 333, DP Sh milioni 3.3, APPT-Maendeleo Sh milioni 11 na Chausta Sh milioni 2.4.
Uchafu
“Ninajua vyama vyenye kelele ni hivi vikubwa vya CCM na Chadema, ambavyo ndio vilitakiwa kuwa mfano lakini ukweli uko wazi, hatuwezi kuwa mabingwa wa kusimama bungeni kushughulikia Serikali kwa matumizi mabaya wakati sisi wenyewe si wasafi,” alisema Zitto.
Alisema Sheria ya Vyama vya Siasa ya 2009 iko wazi kuwa ni wajibu wa CAG kukagua hesabu za vyama vya siasa na kuwasilisha ripoti yake kwa Msajili wa Vyama vya Siasa, ambaye naye anatakiwa atoe ripoti hizo kwenye gazeti la Serikali kila mwaka.
Alifafanua kwamba vyama hivyo vilitakiwa kuteua kampuni ya kufanya ukaguzi lakini kati yao, ni CCM na TLP tu vilivyoteua kampuni za kufanya ukaguzi huo na kupeleka kwa CAG kwa ajili ya uthibitisho, ingawa hata baada ya kuteua kampuni hizo, havikupeleka ripoti kama vilivyopaswa kufanya kisheria.
“Kwa miaka minne mfululizo, hakuna taarifa yoyote iliyomfikia CAG ya ukaguzi wa chama wala kutolewa kwenye gazeti la Serikali, na kwa mujibu wa sheria hiyo kifungu cha 14 (4), Msajili anatakiwa azuie ruzuku kwa chama ambacho kitashindwa kuwasilisha taarifa zake za ukaguzi, hili halijafanyika jamani kwa miaka minne sasa,” alisisitiza.
Alisisitiza kwa vyama hivyo, kuacha kuleta masuala ya ujanja na kuingiza siasa katika eneo linalohusu fedha za umma. “Nasisitiza mimi hapa sifanyi siasa natekeleza sheria, kama ni siasa tukutane kwenye majukwaa, naomba hawa wenzangu waache kubwabwaja huko nje…tuache kuingiza ujanjaujanja linapokuja suala linalohusu fedha za umma, nitaendelea kutetea fedha za umma hata nikinyongwa sijali,” aliapa.
Alionya kuwa Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka, Bunge inaruhusu Kamati kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mtu yeyote atakayeonesha dharau ikiwemo kifungo, hivyo endapo vyama hivyo vitashindwa kuwasilisha ripoti hizo kuna uwezekano wa kuadhibiwa ikiwepo kufungwa.
“Sheria hii inatoa mamlaka kwa kamati kuwachukulia hatua ikiwemo kuwafunga hadi siku saba, namaanisha wakiendelea kubwabwaja wataenda Segerea hadi Ukonga, hapa natekeleza Sheria na si siasa,” alionya.
Kuhusu madai kuwa vyama hivyo havikuwa na fedha za kukagua mahesabu yao, wakati kazi ya ukaguzi ni ya CAG aliyesema hakuwa na fedha za kufanya hivyo, Zitto alisema kauli hiyo ni hizo hizo propaganda, kwa kuwa haiwezekani taasisi yenye mapato madogo kama Bodi ya Tumbaku, haina fedha kama ilizonazo CUF, lakini inafedha za kufanya ukaguzi, CUF isiwenazo.
Umaarufu


Akizungumza kwa hasira baadhi ya majina aliyopewa baada ya kuagiza vyama hivyo vizuiwe kupata ruzuku, alisema wamemuita majina mengi mabaya ikiwemo kudaiwa kuwa anatafuta umaarufu.
“Suala la umaarufu silihitaji kwa kuwa tayari nimeshakuwa maarufu, hao wanaosema, nina uhakika kabisa hakuna aliye maarufu kama mimi,” alisema.
Aliwataka kama kuna anayemzidi umaarufu kati ya waliozungumza kutetea vyama vyao, ajitokeze waende pamoja shule yeyote ya msingi, ili wanafunzi waulizwe nani kati yao na yeye wanayemtambua.
Kwa mujibu wa Zitto, ameamua kulivalia njuga suala hilo kwa kuwa inavyoonekana Msajili na CAG, wanaogopa vyama hivyo kwani taarifa ya mwisho kuwasilishwa kwa Msajili kuhusu ukaguzi ni ya CCM ya mwaka 2008, na hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa kwa mujibu wa Sheria.
Alisema Msajili alipaswa kuzuia ruzuku ya vyama hivyo miaka mitatu iliyopita, na kusisitiza kuwa yeye haogopi mtu ilimradi anasimamia Sheria.
Pamoja na hayo, kwa taarifa ambazo gazeti hili imezipata, Mutungi, jana alikutana na viongozi wa vyama vya siasa kujadili suala hilo, ingawa taarifa ya kilichojadiliwa haikuweza kupatikana.
Madai ya vyama Wakati Zitto akitoa kauli hiyo, Chadema jana iliitisha mkutano wa waandishi wa habari kudai kuwa madai ya PAC sio sahihi na hayana ukweli.
Katibu wa Baraza la Wadhamini ambaye ni Mkurugenzi wa Fedha wa Chadema, Antony Komu alisema taarifa za ukaguzi wa fedha kwa mwaka 2010/2011 na 2011/2012 ilishakabidhiwa huku akionesha barua aliyodai ni ya Msajili wa Vyama vya Siasa yenye kumbukumbu CDA.112/123/01a/37 ya Septemba 4 mwaka 2012 kama uthibitisho.
Naye Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), ya CCM Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, Jumapili iliyopita alisema chama hicho kiko tayari kwenda mbele ya PAC na hesabu zilizokaguliwa na wakaguzi wa nje, Shirika la Ukaguzi la Taifa (TAC).
Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Tanzania Bara, Julius Mtatiro alisema mahesabu yao yako safi, ila wameshindwa kukaguliwa kwa kuwa Serikali haijatoa fedha za kufanya ukaguzi.
Katibu Mkuu wa NCCRMageuzi, Samuel Ruhuza, alisema chama hicho kiko tayari kuwasilisha hesabu zake, ila walishindwa kuwasilisha baada ya kuelezwa kuwa CAG, ndiye aliyepaswa kukagua.

Tuesday, 25 June 2013

MBUNGE SUGU ASHIKILWA NA POLISI

MBUNGE SUGU ASHIKILWA NA POLISI


Hizi ni habari ambazo nimezipokea si muda mrefu sana,Mr ii aka MH. SUGU amekamatwa na polisi leo asubuhi akijiandaa kwenda kwenye kikao cha press talk katika ukumbi wa Balaza la Sanaa la Taifa(BASATA),mpaka sasa haijafahamika sababu za kukamatwa kwa mkongwe huyo wa muziki wa Hiphop nchini..


Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi amegoma kufuta kauli ya kumtukana waziri mkuu na kusema

“Naskia kuwa watu wanasema kwamba eti nimefuta kauli yangu kuhusu waziri mkuu na amri yake kwa polisi kupiga wananchi?!

Sina sababu ya kufuta wala kuomba radhi, na nasimamia kauli yangu to the end…Kwanza ‘upumbavu’ sio tusi, upumbavu kwa kiingereza ni stupidity-which is lack of knowledge and understanding…

So hata uwe na cheo gani kama ukishindwa kuwa na ‘understanding’ juu ya madhara ya kauli zako kwa taifa then u r ‘stupid’…ambapo kwa kiswahili ndio ‘mpumbavu’
 


Pamba kali toka mwaip fashion Tabata



KWA DADAZ WAENDAO NA WAKATI....NA WENYEKUPENDA KUPENDEZA


Add caption




Monday, 24 June 2013

HAPA MPAKA KIELEWEKE! (JOYCE KIRIA) AMTAKA MUMEWE

 BAADHI YA PICHA ZIKIMWONYESHA MTANGAZAJI JOYCE KIRIA
AKILILIA HAKI YAKE YA MSINGI

 Mtangazaji wa televisheni ya Chanel 5 EATV Joyce Kiria akiwa amewashikilia watoto wake Lingatone Kileo kulia na Lincorn wakati alipozungumza na waandishi wa habari katika mtaa wa Samora na kupaza sauti kuomba msaada kwa Rais Jakaya Kikwete na watanzania kwa ujumla ili kusaidiwa na kujua aliko mume wake Henry Kileo ambaye inadaiwa amepelekwa Igunga akituhumiwa na kesi huko Joyce Kiria amesema mpaka sasa hajaambiwa kama mume wake yuko wapi hivyo hata kama ana makosa anaomba afahamishwe kwani hajui kinachoendelea mpaka sasa

MNYAMA SOGY DOGY ATINGISHA GETI LA CHADEMA

Nguli wa muziki wa kizazi kipya Soggy Doggy Anter aka Anselm Tryphone Ngaiza leo ametangaza nia ya kugombea Ubunge wa jimbo la Segerea, Dar es Salaam kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, MWAKA 2015.

Msanii huyo ametiririka katika ukurasa wake wa facebook, na hapa nanukuu "Shikamoo Mbunge wa Segerea, Makongoro Mahanga, imetosha sasa nadhani ni zamu yangu kuwatumikia wana-segerea 2015 kupitia CHADEMA" mwisho wa kunukuu. Pia kwenye ukurasa wake wa twitter imesomeka ivyo ivyo.

 Msanii huyu amesema ameamua kufanya ivi ili kuwasaidia na kuwaletea maendeleo wana-segerea na watanzania kiujumla.

Pia  ameamua kugombea kupitia CHADEMA, kwasababu ndo chama kinachoweza kufanya mabadiliko kwenye jamii kwasasa.

Nikamuuliza je amemfuata rafiki yake Joseph Mbilinyi aka "SUGU" katika chama icho, akasema hapana, hawajawahi kupewa ushawishi wowote wa kisiasa na Nguli huyo wa muziki wa Hip Hop.

Wana-Segerea kazi kwenu kijana ameamua na amedhamiria

Thursday, 21 March 2013

MOUNT KILIMANJARO



The origin of the name "Kilimanjaro" is not precisely known, but a number of theories exist. European explorers had adopted the name by 1860 and reported that "Kilimanjaro" was the mountain's Kiswahili name.[6] But according to the 1907 edition of The Nuttall Encyclopædia, the name of the mountain was "Kilima-Njaro".[7]

Johann Ludwig Krapf wrote in 1860 that Swahilis along the coast called the mountain "Kilimanjaro". Although he did not support his claim,[8] he claimed that "Kilimanjaro" meant either "mountain of greatness" or "mountain of caravans". Under the latter meaning, "Kilima" meant "mountain" and "Jaro" possibly meant "caravans".[6]

Jim Thompson claimed in 1885, although he also did not support his claim,[8]

The term Kilima-Njaro has generally been understood to mean the Mountain (Kilima) of Greatness (Njaro). This is probably as good a derivation as any other, though not improbably it may mean the "White" mountain, as I believe the term "Njaro" has in former times been used to denote whiteness, and though this application of the word is now obsolete on the coast, it is still heard among some of the interior tribes. Either translation is equally applicable.... By the Wa-chaga[,] the mountain is not known under one name, the two masses which form it being respectively named Kibo and Kimawenzi.[9]

According to a website owned by the Jet Propulsion Laboratory, "Kilima" is an ancient Kiswahili word for "shining".[10] Similarly, Krapf wrote that a chief of the Wakamba people, whom he visited in 1849, "had been to Jagga and had seen the Kima jaJeu, mountain of whiteness, the name given by the Wakamba to Kilimanjaro...."[11] More correctly in the Kikamba language, this would be Kiima Kyeu, and this possible derivation has been popular with several investigators.[8]

Others have assumed that "Kilima" is Kiswahili for "mountain". The problem with this assumption is that "Kilima" actually means "hill" and is, therefore, the diminutive of "Mlima", the proper Kiswahili word for mountain. However, "[i]t is ... possible ... that an early European visitor, whose knowledge of [Kiswahili] was not extensive, changed mlima to kilima by analogy with the two Chagga names; Kibo and Kimawenzi."[8]

A different approach is to assume that the "Kileman" part of Kilimanjaro comes from the Kichagga "kileme", which means "which defeats", or "kilelema", which means "which has become difficult or impossible". The "Jaro" part would "then be derived from njaare, a bird, or, according to other informants, a leopard, or, possibly from jyaro a caravan."

According to one [Wachagga] informant, the old men tell the story that long ago the Wachagga, having seen the snowy dome, decided to go up to investigate; naturally, they did not get very far. Hence the name: kilemanjaare, or kilemanyaro, or possibly kilelemanjaare etc.- "which defeats," or which is impossible for, the bird, the leopard, or the caravan. This is attractive as being entirely made up of [Wachagga] elements based on an imaginable situation, but the fact remains that the name Kilimanjaro is not, and apparently never has been, current among the Wachagga as the name of the mountain. Is this then only, as other Wachagga suggest, a latter-day attempt to find a [Wachagga] explanation when pressed to do so by a foreign enquirer? Is it perhaps arguable that the early porters from the coast hearing the Wachagga say kilemanjaare or kilemajyaro, meaning simply that it was impossible to climb the mountain, imagined this to be the name of the mountain, and associated it with their own kilima? Did they then report to the European leaders of the expedition that the name of the mountain was, their version of the Kichagga, which, further assimilated by the European hearer, finally became standardised as Kilimanjaro?[8]

In the 1880s, the mountain became a part of German East Africa and was called "Kilima-Ndscharo" in German following the Kiswahili name components.[12] L

When on 6 October 1889, Hans Meyer reached the highest summit on the crater ridge of Kibo, he named it "Kaiser-Wilhelm-Spitze" ("Kaiser Wilhelm peak").[13] That name apparently was used until Tanzania was formed in 1964,[14] when the summit was renamed "Uhuru", meaning "Freedom Peak" in Kiswahili.[15] The Kaiser Wilhelm-Spitze with its altitude of 5895 meters was known at that time as the highst mountain of the German Empire.